Tuesday, February 5, 2013

Mwasiti afunguka kuhusiana na mali anazomiliki!!


Hitmaker wa Nalivua Pendo na Mapito, Mwasiti Almas ameelezea mafanikio aliyoyapata kupitia kazi yake ya muziki ambapo amefanikiwa kununua gari lenye thamani ya milioni 16 na mjengo anaoumalizia maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Kupitia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Mwasiti alisema nyumba hiyo yenye vyumba vitano inatarajiwa kumalizika baada ya miezi michache ijayo.

No comments:

Post a Comment