Tuesday, February 5, 2013

Zola D kuanzisha kipindi cha TV cha mazoezi!



Hivi karibuni Bongo5 ilichat na rapper na bondia nchini Tanzania, Zola D ambaye alisema ana mpango wa kuanzisha kipindi cha TV.

“Now nina mpango wakuanzisha kipindi cha TV pia na kurusha video zangu za mazoezi kwenye Youtube ili kila mtu alie nyumbani aweze kufanya mazoezi sio mpaka uingie gym, “ alisema Zola.

“Mimi siendi gym kufanya mazoezi nafanya home pia gym naenda kama nina game ya boxing,ili niweze kufundishwa na mwalimu mbinu mbali mbali za mapigano na ushindi.”
Zola akiwa na P-Funk

Akijibu swali la ni vipi ameweza kuujenga mwili wake kiasi hicho, Zola amesema, “Mwili wangu nimeujenga toka miaka mingi sana sasa nina miaka 18 tokea nimeanza kufanya mazoezi ndio maana unaweza kuona mwili wangu umejengeka sana kuliko watu wengine hapa Bongo. Pia mazoezi ninayofanya ni mazoezi ya mapigano na mazoezi ya kujenga nguvu kama push up kukimbia,kuruka kamba,na kufanya swimming sababu napenda sana mazoezi na ndio starehe yangu kubwa,pia nafanya mazoezi kila siku ndio chakula cha maisha yangu,so kila siku nazidi kugain na kuongezeka.”

“Mazoezi yananisaidia sana kwenye afya yangu coz sijaumwa malaria huu ni mwaka wa 4 pia mafua kifua nk,coz ukifanya mazoezi damu inakuwa na nguvu sana,”aliongeza.

Hata hivyo Zola amesema hana pambano lolote hivi karibuni na kuongeza kuwa mchezo wa ndondi kwa Tanzania haulipi.

“Game za Bongo hakuna pesa kabisa ni kuumizana tu promoter wenyewe njaa tu, promoter hana hata baiskeli. Nia yangu ni kupigana ngumi za nje na kuitangaza Tanzania.Nipo tayari kupigana na bondia yoyote mkubwa wa dunia coz najua nina kipaji cha sports pia napenda sana kupigana nikitoka damu ndio naskia raha sana najiona mimi ndio mwanaume.”
Zola na Mad Ice


Kuhusu kuzichapa kiukweli na Mad Ice ambaye pia ni bondia na ameigiza kwenye video yake ya Knock OUT, Zola amesema Ice ni mtoto mdogo.

“Mad ice hawezi kupigana na mimi,pia mimi ni mwalimu wake namfundisha boxing. Nawaomba watanzania wazidi kuniombea dua niweze kutimiza ndoto zangu za kupigana level za kimataifa,muziki wangu level za kimataifa na michezo yangu mingine kama kukimbia mita 100, mita 200,kuruka viunzi,kucheza rugby, kupigana boxing mixed martial arts.”

Video ya Me & You ya Ommy Dimpoz ft. Vanessa Mdee kuzinduliwa Feb 10, Maisha Club



Jumapili hii ya February 10, Omary Nyembo aka Ommy Dimpoz ataizindua rasmi video ya wimbo wake Me and You aliomshirikisha Vanessa Mdee. Video hiyo imefanywa na Ogopa Dj’s wa nchini Kenya.

Katika uzinduzi huo utakaofanyika New Maisha Club, Ommy atasindikizwa na wasanii wenzake wakiwemo Diamond,Dully Sykes,MwanaFA na performance kutoka kwa wasanii wakali wa Africa Mashariki.

Prezzo na Goldie kufunga ndoa February 9



Kwa mujibu wa mitandao mbalimbali nchini Nigeria, rapper Jackson Makini aka Prezzo anatarajia kufunga ndoa na mwanamuziki wa Nigeria Goldie February 9.

Habari hiyo pia imeandikwa na website ya Big Brother Africa. Harusi hiyo itafanyika jijini Lagos, Nigeria.

Katika hatua nyingine mwakilishi wa mwaka jana wa Nigeria kwenye shindano la Big Brother Africa, anatarajia kuanzisha Reality TV show yake.Goldie anaanzisha show hiyo iitwayo ‘Tru Friendship’. ‘Tru Friendship’ itaonesha maisha ya kila siku ya muimbaji huyo wa Skibobo, Goldie, yote kama mtu maarufu na kama Susan Harvey.

Show hiyo itaanza kuonekana mwishoni mwa mwe

Mwasiti afunguka kuhusiana na mali anazomiliki!!


Hitmaker wa Nalivua Pendo na Mapito, Mwasiti Almas ameelezea mafanikio aliyoyapata kupitia kazi yake ya muziki ambapo amefanikiwa kununua gari lenye thamani ya milioni 16 na mjengo anaoumalizia maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

Kupitia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM, Mwasiti alisema nyumba hiyo yenye vyumba vitano inatarajiwa kumalizika baada ya miezi michache ijayo.