Tuesday, January 29, 2013

Picha: Timbulo na Rose Ndauka waigiza filamu iitwayo “World of Benefit”




Msanii mahiri wa muziki wa Bongofleva nchini, Ally Timbulo, ameanza safari mpya kwenye tasnia ya filamu kwa kushoot filamu na Rose Ndauka akiwa kama ni mhusika mkuu. Filamu hiyo inaitwa World of Benefit.

Ndani ya filamu hiyo Timbulo anakuwa ni kijana anaye onyesha mapenzi ya kweli kwa Rose aliyeolewa. Waigizaji wengine kwenye filamu hiyo ni pamoja na Mohamed Olutu ‘Mzee Chilo’, Mama Mjata, Hemed Suleiman ‘Phd’, na Awadhi Saleh muigizaji anayekuja juu katika tasnia ya filamu nchini.

“Nimepata bahati kufanya kazi na wasanii wakongwe kwahiyo ni kitu cha kujivunia na pia mimi ni mhusika mkuu kwenye hii filamu ambapo Rose Ndauka kaolewa katika ndoa ya mke zaidi ya mmoja. Rose yupo nyumba ndogo kwahiyo nyumba aliyopewa na bwana wake ananiita niishi naye kwakuwa mimi ni mpenzi wake wa muda mrefu kwahiyo namwonyesha “True Love” na tunapendana sana na yule bwana wake tunamfanya kama mwezeshaji wa maisha yetu” anasema Timbulo.

Rose-Ndauka-Timbulo-Ali

Seleman-mkangara-Mapunda-Selles

Filamu ya World of Benefit imetayarishwa na mtayarishaji wa filamu Hamees Suba ‘Kemikali’ na inaongozwa na Selles Mapunda ‘Director of Directors’, akisaidiwa na Suleiman Mkangara ‘Striker’ kwa upande wa upigaji picha wapo wataalamu kutoka Bollywood chini ya kampuni ya Pilipili Entertainment ya jijini Dar es Salaam.

Picha: Filamu Central

Ukata: Malawi yaipiga mnada ndege ya Rais

Serikali ya Malawi leo imetangaza kuwa inaiuza ndege ya Rais wa nchi hiyo Joyce Banda katika jitihada zake kukusanya mapato inayoyahitaji.Ndege hiyo yenye miaka 15, nzima NA inauzwa kwa dola milioni 13.3.

Ndege hiyo ni aina ya Dassault Falcon 900EX, imetengenezwa mwaka 1998 na ina seats 14.Rais wa zamani wa Malawi hayati Bingu wa Mutharika aliinunua ndege hiyo miaka mitano iliyopita licha ya nchi hiyo kukabiliwa na umaskini mkubwa.

Kipindi hicho Mutharika alisema ndege hiyo ilikuwa rahisi kuihudumia licha ya nchi hiyo kutegemea misaada ya karibu nusu ya bajeti yake.

Police investigate shooting on Las Olas Boulevard

Risasi 20 zamkosa Rick Ross! Nani anataka kumuua?



Rick Ross ana bahati kuwa hai.Teflon Don huyo jana amekikwepa kifo baada ya mtu asiyejulikana kuishambulia kwa risasi gari yake aina ya Rolls-Royce alipokuwa barabarani huko Fort Lauderdale, Miami asubuhi ya jana.

Polisi wa Ft. Lauderdale wamedai kuwa tukio hilo lilitokea mida ya saa 11 alfajiri ambapo Ross alikuwa amekaa nyuma ya Rolls Royce hiyo yenye rangi ya silver.Baada ya kusikia risasi hizo, mamlaka zinasema Ross na mtu waliyekuwa naye aitwaye Shateria L. Moragne walijaribu kukwepa lakini alijikuta akikosa control na kwenda kugonga jingo.
WSVN-TV -

Kwa mujibu wa gazeti la Miami Herald, Ross alikuwa ametoka kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutumiza miaka 37.
Hakuna aliyeumia kwenye tukio hilo.

Polisi bado hawajapata sababu za mtu huyo kutaka kumuua Rick Ross ambapo mashuhuda wanadai jumla ya risasi 20 zilipigwa na hakuna hata moja iliyoifikia gari hiyo.Hata hivyo Herald limedai kuwa risasi kadhaa zilipiga majengo ya karibu ikiwemo moja iliyopiga dirisha la mgahawa ambao Rick Ross alikuwa ametoka kula.

Mwishoni mwa mwaka jana Ross alisitisha tarehe ya ziara yake kufuatia vitisho vya kuuawa.