Thursday, January 31, 2013

Rihanna afunguka kwenye jarida la Rolling Stone sababu za kumpa Chris Brown ‘second chance’



Rihanna amefunguka mengi kuhusu uhusiano wake na Chris Brown na kuweka wazi kwanini aliamua kumpa second chance.

“Niliamua ilikuwa muhimu zaidi kwa mimi kuwa na furaha, “ aliliambia jarida lijalo la Rolling Stone. “Sikutaka kuacha mtazamo wa mtu yeyote hata kama ni kosa, ni kosa.”

Katika toleo hilo litakalotoka kesho, Rihanna ameelezea vitu vilivyobadilika kati yao.

“Unatuona tukitembea sehemu, tukiendesha sehemu, tukiwa studio, tukiwa club, na unadhani unajua. Lakini ni tofauti sasa. Hatuna majibizano kama ya zamani tena. Tunaongea kuhusu mambo. Tunathaminiana. Tunajua fika tunachokataka sasa na hatutaki tukipoteze.”

Picha: Uchukuaji video ya wimbo mpya wa MwanaFA ft. Kilimanjaro Band & Mandojo na Domokaya


Uchukuaji picha wa video ya wimbo mpya wa rapper Hamis Mwinjuma aka MwanaFA aliyoishirikisha bendi kongwe ya Kilimanjaro Band aka wananjenje na Mandojo na Domokaya umeanza rasmi leo jijini Dar es Salaam chini ya director Karabani.

“Karabani anaishoot hii video lakini inapelekwa South Africa kama ilivyoripotiwa na watu wa God Father ndio wanaedit hii video na sababu yangu ilikuwa ni kwamba ningekuwa nimefanya peke yangu ningeenda kuifanya South Africa lakini una band, una watu sita, saba una Mandojo na Domo Kaya watu tisa na mimi ni wa kumi, wimbo mmoja ungenitia umaskini hapo hapo, yaani naweza kufanya lakini ningeumwa mpaka mwezi wa sita,” amesema MwanaFA. “Kwa gharama zilivyo tukaona hakuna sababu jamaa wanasema mara nyingi hata sisi tunapata picha nzuri tatizo linakuja kwenye editing. Vitu hivi pia vina politics, watu wanatumia connections walizonazo, Godfather akifanya una uhakika wa kwenda Trace, una uhakika wa kwenda MTV Base una uhakika wa kwenda Channel O kama kawa yaani.”

Akizungumzia sababu za kuichagua band ya Kilimanjaro FA amesema, “ Unajua suala ni kwamba unatafuta angle tofauti, sijakaa kwenye muziki kwa miaka 12 for no good reason yaani kulikuwa na sababu ya mimi kubaki na kwasababu natafuta angle mpya kila siku ya kutokea. Sijawahi kujisikia vizuri kuperform nyimbo yangu kama nilivyojisikia wakati naperform na Njenje kwahiyo nikaona hawa ndio band ambayo nataka kuitumia Plus Njenje ina miaka 42 inafanya muziki kwahiyo kama unataka kutengeneza picha ya ulegendary lazima kila kitu kiwe na picha hiyo, siwezi kuchukua bendi za watoto wadogo wakati bendi ya malegendary ipo.”

Aidha MwanaFA amesema anashow inakuja hivi karibuni aliyoipa jina la The Finest na atakayoshirikiana na bendi hiyo pamoja na wasanii aliowahi kuwashirikisha kwenye nyimbo zake. “The Finest iliripotiwa kama wimbo lakini The Finest actually ni show sio wimbo. Ni show ya mara moja, hatutaki kuifanya sana itakuwa ni kitu kinachozoeleka, sio ya watu wengi ni show wanayohudhuria watu kama 500, corporate show. Tunachojaribu ni kuuvusha muziki, unajua aina ya muziki tunaoufanya mara nyingi unaonekana ni muziki wa watu fulani.

Kilichobaki ni kwamba huu muziki unahitaji hela na unahitaji hela kutoka kwenye corporations na sio hata mauzo ya muziki. Corporations zinatakiwa ziweke hela kwenye muziki na namna ambayo tunatakiwa kuzishawishi kufanya hivyo ni kwa kuwaonesha kwamba muziki wetu una nguvu kiasi gani, muziki wetu ni mzuri kiasi gani na ndio hiyo idea ya The Finest ilipokuja.”

Hizi ni baadhi ya picha za uchukuaji wa video hiyo.
Magdalena na MwaJ wa True Eyes Modeling Agency watakaotumika kwenye video hiyo


Mpiga saxophone wa Kilimanjaro Band


Ray of Hope ya Pastor Myamba yatajwa kuwania AfricaMagic Viewers’ Choice Awards (AMVCAs)



Filamu ya kitanzania ya Ray of Hope imetajwa kuwania tuzo za kwanza za AfricaMagic Viewers’ Choice Awards zitakazotolewa tarehe 8 na 9 March, 2013 huko jijini Lagos, Nigeria.

Ray of Hope imetajwa kwenye kipengele cha BEST LOCAL LANGUAGE MOVIE (SWAHILI) na inashindana na filamu zingine za Sakalakata na Zeinabu.

Katika filamu hiyo waigizaji walioigiza ni pamoja na Pastor Myamba, Baby Madaha, Hashim Kambi na wengine.

Hii ni orodha nzima ya majina yalitotajwa kuwania tuzo hizo:

BEST ACTRESS IN A DRAMA
Man on Ground | Bubu Mazibuko
The Mirror Boy | Genevieve Nnaji
Otelo Burning | Nolwazi Shange
Maami | Funke Akindele
Perfect Picture | Jackie Appiah

BEST ACTRESS IN A COMEDY
The Return of Jenifa | Funke Akindele
Clinic Matters | Lilian Esoro
Dumebi the Dirty Girl | Mercy Johnson

BEST ACTOR IN A DRAMA
Jacob’s Cross | Fabian Adeoye Lojede
Two Brides and a Baby | O.C Ukeje
Down & Out | Kenneth Uphopho
The Mirror Boy | Edward Kagutuzi
Otelo Burning | Jafta Mamabolo

BEST SUPPORTING ACTOR
Man on Ground Fabian Adeoye Lojede
The Mirror Boy Osita Iheme
Otelo Burning Thomas Gumede
A Good Catholic Girl Matthew Nabwiso
Two Brides and a Baby Kalu Ikeagwu

BEST ACTOR IN A COMEDY
House a Part | Hafiz Oyetoro
Glorious Journey | Kunle Bamtefa
The Bovi Ugboma Show | Bovi Ugboma
Clinic Matters | Francis Odega
Wanna Be | Ikhide Isaac

BEST SUPPORTING ACTRESS
Man on Ground | Thishiwe Ziqubu
Otelo Burning | Harriet Manamela
Akun | Regina Chukwu
Old Cargo Young Blood | Taiwo Atigogo
Lies that Bind | Maureen Koech

BEST COSTUME DESIGNER
The Mirror Boy | Ngozi Obasi
Perfect Picture | Jayne Awoonor-Williams
Two Brides and a Baby | Frank Osodi Richard
Kawanu | Preston Mwila
Spider | Nkiru Nwauzor

BEST SHORT FILM
Big Daddy | Christopher Ihidero
Yellow Fever | Ngendo Mukii
Down & Out | Udoka Oyeka

BEST WRITER (COMEDY)
Skeem | Tim Greene
Perfect Picture | Shirley Frimpong-Manso
Clinic Matters | Paul Igwe
The Bovi Ugboma Show | Bovi Ugboma
Wanna Be | Teru Ekuerhale

BEST SOUND EDITOR
Man on Ground | Michael Botha & Joel Assaizky
Otelo Burning | Juli vanden Berg & Tiago Correia-Paulo
The Mirror Boy | Obi Emelonye
Perfect Picture | Elorm Adablah
A Sting in a Tale | Elorm Adablah

BEST MOVIE DIRECTOR
Skeem | Tim Greene
Man on Ground | Akin Omotoso
The Mirror Boy | Obi Emelonye
Otelo Burning | Sara Blecher
Perfect Picture | Shirley Frimpong-Manso

BEST LIGHTING DESIGNER
Otelo Burning | Dave Howe
Two Brides and a Baby | Eleazu Texas
Maami | Oluwole Olawoyin
Down and Out | Terry Emmanuel
Perfect Picture | Ken Attoh

BEST ART DIRECTOR
Maami | Bola Belo
Lies that Bind | Carol Mbugua
Kawanu Bernard | H. Mulenga
Two Brides and a Baby | Blessing Effiom Egbe
Otelo Burning | Anita van Hemert & Chantel Carter

BEST MOVIE (OVERALL)
Skeem | Tim Greene
Man on Ground | Akin Omotoso/Fabian Adeoye Lojede/Hakeem Kae-Kazim/Rosie Motene
Jozi King | Jamie Ramsay
Otelo Burning | Sara Blecher
The Mirror Boy | Obi Emelonye

BEST PICTURE EDITOR
Otelo Burning | Megan Gilli
Man on Ground | Aryan Kaganof
Two Brides and a Baby | Shola Ayorinde
Lies that Bind | Reg Chuhi & Kevin Ireri
Clinic Matters | Kayode Afolabi

BEST MOVIE (COMEDY)
Skeem | Tim Greene
Wisdom of Thomas Collins | Chinedu Ezenwa
Phone Swap | Kunle Afolayan
The Return of Jenifa | Funke Akindele
Open Fire 2 | George Edmund

BEST MOVIE (DRAMA)
Man on Ground | Akin Omotoso/Fabian Adeoye Lojede/Hakeem Kae-Kazim/Rosie Motene
The Mirror Boy | Obi Emelonye
Otelo Burning | Sara Blecher
Adams Apple | Ken Attoh
A Sting in a Tale | Ken Attoh

BEST LOCAL LANGUAGE MOVIE (YORUBA)
Maami | Tunde Kelani
Akun | Regina Chukwu
Gbajumo Oladipo | Ariyeke

BEST LOCAL LANGUAGE MOVIE (HAUSA)
Asirka | Aminu Abdullahi/Hafizu Bello
Yunkuri | Aminu Abdullahi
Faida Nura | A. Ali/Hafizu Bello

BEST LOCAL LANGUAGE MOVIE (SWAHILI)
The Ray of Hope | Sameer Srivastava/Sanjni Srivastava
Sakalakata | Henry Lenga
Zeinabu | Rudi Nyumbani Quentin Hughes/Alex Konstantaras

BEST WRITER (DRAMA)
Otelo Burning | James Whyle/Sara Blecher/The Cast Workshop
The Mirror Boy | Obi Emelonye/Amaka Obi-Emelonye
Two Brides and a Baby | Blessing Egbe
A Sting in a Tale Shirley | Frimpong-Manso
Perfect Picture | Shirley Frimpong-Manso

BEST TELEVISION SERIES
The XYZ Show | Godffrey Mwampembwa/Marie Lora-Mungai
Peep | Ken Attoh/Shirley Frimpong-Manso
Jozi Moving the City | Lance Stehr
DemiGods | Benjamin Odiwuor Abonyo
Makutano Junction | Patricia Gichinga/David Campbell

BEST CINEMATOGRAPHER
The Mirror Boy | Clive Norman
Skeem | Tom Marais
Man on Ground | Paul Michelson
Otelo Burning | Lance Gewer
Maami | Sarafa Abagun

BEST MAKE-UP ARTIST
Otelo Burning | Jacqui Bannermen
The Mirror Boy | Gabriel Okorie
Tales of Eve | Biola Poopola
Perfect Picture | Jayne Awoonor-Williams
Kawanu | Christin Ngoma

Waziri (Njenje): Muziki wa Tanzania umekua kibiashara lakini unakufa kitaaluma



Muimbaji mkongwe wa Kilimanjaro Band aka Wana Njenje Waziri Ally amesema muziki wa Tanzania umekua sana kibiashara lakini unaendelea kufa kitaaluma.

Akiongea na Bongo5, Mzee Waziri ambaye ni kiongozi wa bendi hiyo kongwe nchini Tanzania amesema kwa sasa muziki unafanyiwa promotion sana na hivyo kuufanya uuzike. “People are making money sasa hivi sio kama sisi tulivyoanza muziki wakati huo,” alisema. “Na ndio maana sasa unaona mfumko wa wanamuziki wapya ni wengi sana kila mmoja anajua akitoa wimbo mpya atapata hela yake atanunua gari, atanununua nyumba nk. Kwahiyo kibiashara unakua lakini sio kitaaluma, taaluma ya muziki inakufa. Kwasababu kila miaka inavyozidi kwenye wanamuziki wanapungua, nikisema wanamuziki naamanisha wale wanaojua taaluma ya muziki, either amekwenda shule kusoma muziki au anapiga tu muziki bila kusoma ama kwa kipaji lakini anapiga muziki kiusahihi.”:

Waziri amesema wanamuziki wa sasa wanapenda njia za mkato kutoka hali inayochangia kwa kiasi kikubwa taaluma ya muziki kushuka ama kufa na kuongeza kuwa Tanzania kwa sasa imeachwa nyuma na nchi zingine za Afrika Mashariki hususan Uganda.

“Music imehamia Uganda, ukisikiliza production za Uganda utasikia kuna watu wametuliza akili zao wamefanya arrangement na kuna music ndani yake, ukisikia uimbaji wa Uganda wanaimba, unajua kabisa hapa kuna waimbaji.”

Matumaini (mchekeshaji) azidiwa akiwa Msumbiji, avimba miguu na tumbo, anahitaji msaada



Mchekeshaji na muigizaji wa Tanzania Tumaini Martin ‘Matumaini’ yupo nchini Msumbiji ambako anasumbuliwa na tatizo la kuvimba tumbona miguu na mwili kukosa nguvu. Kutokana na hali hiyo muigizaji huyo anahitaji msaada wa nauli ili aweze kurudi na kuja kupata matibabu nchini.

THE BIG DAD imepata taarifa rasmi kutoka kwa mwenyekiti wa chama cha waigizaji taifa Michael Sangu aliyesema, “Msanii mwenzetu Matumaini anaumwa sana na bado mpaka sasa yupo Msumbiji na kitu ambacho kinamsumbua zaidi ni kuvimba tumbo na miguu na akiwa hana uwezo wa kujitibia wala nauli ya kuweza kurudi nchini”.

Taarifa za awali zinasema kuwa Matumaini aliingia nchini Msumbiji katika ziara ya kisanii akiwa huko alimpata jamaa akaamua kufanya maisha yake huko. Wenzake aliosafiri nao kwenda nchini humo Tanzania na yeye kuanza maisha mapya.

Kwa wale wanaopenda kumsaidia wanaweza kuwasilisha michango yao kutuma kupitia tigo pesa kwa namba 0718 951 355 kwa mwenyekiti Mike Sangu.

YOTE KWA HISANI YA BONGO5