Monday, October 15, 2012

ZAMBI AWA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MBEYA




Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mashariki Godfrey Zambi ameshinda nafasi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa

WEMA SEPETU NA AUNT EZEKIEL WAOMBA RADHI KWA PICHA ZAO MBAYA ZA FIESTA



Waigizaji wa filamu nchini Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wamewaomba radhi watanzania kwa picha zao mbaya walizopigwa kwenye show za Fiesta.


Wasanii hao wamezungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa habari maelezo jijini Dar es Salaam kwaajili ya kuomba radhi kwa kupigwa picha hizo za nusu utupu walizopigwa kwenye show hizo.

Wakiongena waandishi wa habari Aunty Ezekiel amesema ameumizwa na kitendo hicho kwakuwa wao kama wanawake katika jamii, wana wazazi, ndugu jamaa, marafiki pamoja na mashabiki wao wanaowapenda na kuwaheshimu.

Hivi karibu Aunty Ezekiel alijitetea na kunukuliwa kwenye chanzo kimoja akisema, “Ni kweli nilikuwa ninacheza katika Jukwaa (Stage) na nilikuwa nimekunywa, lakini sikuwa nimedhamiria kukaa uchi bali ni mbinu za wapiga picha ambao walitumia njia ya kuamua kunidhalilisha kwa kunipiga picha wakiwa chini ya Jukwaa (Stage) ili wapate kuuza magazeti yao, hata ukiangalia picha zenyewe zimepigwa kiujanja sana.”

Waigizaji hao waliongozana na katibu Mkuu wa shirikisho la filamu Tanzania, TAFF, Wilson Makubi.



STAMINA KUJA NA ALBAM YENYE NYIMBO 20


Amesema nyimbo nyingi katika albam hiyo zitakuwa na ujumbe wa kijamii yaani conscious zaidi.

Aliongeza kuwa pamoja na kuwepo kwa nyimbo zake zilizotoka kama Kabwela, Alisema na Najuta Kubalehe, katika albam hiyo kuna wimbo aliomshirikisha Fid Q ambaye anamchukulia kama baba yake kisanaa katika wimbo uitwao Like Father Like Son.

Fid pia atalipia gharama zote za kufanyika kwa video mpya ya Stamina ambayo hakutaja ni ya wimbo gani.

TANZANIA NAYO YAJIPANGA KUZIZIMA SIMU BANDIA


Tanzania inatarajia kuchukua hatua kama iliyochukuliwa nchini Kenya ya kuzichinjia baharini simu zote za bandia ambazo nyingi ni za kichina kwa kuzizima kabisa.


Taarifa hiyo imetolewa na kaimu meneja mawasiliano wa mamlaka ya mawasiliano (TCRA) Semu Mwakyanjala ambaye amesema mamlaka hiyo itaanza kwa kutoa elimu kwa umma kuhusiana na umuhimu wa kununua simu halali.

Ameliambia gazeti la Daily News Jumapili kuwa hatua hiyo itachukuliwa na nchi zote wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki zikiwemo Rwanda, Uganda na Burundi.

Kuna taarifa kuwa makampuni mengi ya simu nchini Tanzania yameupokea mpango huo kwa shingo upande kwa hofu kuwa yatapoteza wateja wengi.

Kwa upande wa tume ya mawasiliano ya Uganda (UCC) hatua hiyo ya kuzima simu bandia itafanyika mwishoni mwa mwezi November.