Thursday, January 24, 2013

Ball Player: Izzo B akumbushia alikotoka, mafanikio na jinsi wasanii wa zamani ‘wanavyohate’


Leo hii rapper kutoka Mbeya Emmanuel Simwinga aka Izzo B, ameachia ngoma mpya iitwayo Ball Player akiwa na Quick Rocka na Ngwair.

Beat ya ngoma hii imetengenezwa na Nahreel na nirahisi kusikia touch za kipekee za beatmaker huyo hasa zile brass zinasosikika vizuri kwenye chorus iliyoimbwa na Quick Rocka pamoja na zile drums zinazosikika kama zimepigwa live, design kama beat za Just Blaze. Lamar ndiye aliyemalizia vocals na mixing.

Katika verse ya kwanza ya Ball Player, Izzo B anazungumza jinsi alivyotoka mbali kwa kuja Dar kuifuata ndoto yake ya muziki na kufikia kwa washkaji. “Nimekuja Dar sina ghetto ila now naishi kwangu,” anasema na kuzungumzia jinsi mambo yalivyo safi sasa hivi.

Verse ya pili anaingia Ngwair na kama kawaida yake swagga zinakuwa on. “Mi nahustle hard ndio swagga zangu everyday, Big Beats zinahit kwa streets bila Dre”.Anazungumzia jinsi ambavyo muziki anaudai na wala hashtushwi na watu wanavyomponda.“Usiongeongee hizi dis.com nilishazizoea, unaweza kupaka unavyotaka mimi sijali ukininyea”

Verse ya pili Izzo anarejea na anaendelea na tambo na kisha kuwachana wasanii wakongwe. “Salute kwa kaka zetu japo wachache wenye love, Hawatupendi sisi wa sasa kumbe kisa cha kipumbavu.

Televisheni ya taifa ya Nigeria yazipiga marufuku ‘Alingo’ ya P-Square na Skibobo ya Goldie ft. AY



Shirika la utangazaji la Nigeria, NBC, limezipiga marufuku video nane za wasanii wa Nigeria kwa kile ilichokisema zinaonesha uchezaji wenye matusi (erotic dance).

Video zilizopigwa marufuku ni pamoja na Alingo ya P-Square, Skibobo wa Goldie aliomshirikisha AY na Shake wa Flavour.

List nzima a nyimbo zilizopigwa marufuku na NBC:

1. Tillaman ft Vector- Ma Roll (contains Intimate and suggestive dance steps)
2. Wande Coal – Go Low (scenes of nuditiy in the video)
3. D’Prince – Take Banana (contains Intimate, vulgar, words and suggestive dance steps)
4. Flavour – Shake (vulgar and suggestive dance steps)
5. Goldie – Ski bo bo (features minor with suggestive and immoral dance steps)



6. Chuddy K – Chop My Dollar (features ladies and children with suggestive and Intimate dance steps
7. Timaya – Shake Ur Bum Bum (Intimate, suggestive dance steps with vulgar lyrics
8. P Square – Alingo (Intimate dance scenes at the end of the musical video)

Diamond Platnumz kahamishia penzi kwa Penny? (Picha ndani)



Diamond Platnumz ataendelea kuwa newsmaker kuliko msanii yeyote Tanzania. Hauwezi kupita mwezi bila kuibuka kitu kitakachomfanya aandikwe tena na tena. Katika picha iliyowekwa kwenye ukurasa wa Facebook wa msichana aitwaye Skyner Ally kuna picha inayomuonesha Diamond akiwa amelala usingizi wa pono na msichana anayedaiwa kuwa ni mtangazaji wa DTV, Penny Mungilwa aka Vj Penny. Picha hii inajieleza yenyewe kwa pozi walilolaa kuwa ni wapenzi ama ni one night stand? Wonders will never cease!! Ingia ndani kuona picha hiyo.




Hata hivyo tulipowasiliana na Penny alisema hiyo ni picha iliyopigwa walipokuwa kwenye scene ya movie wanayoigiza pamoja ambayo amesema hana uhakika lini itatoka! Penny na Diamond in a movie? If it’s true then tunaingojea kwa hamu!!

Shaggy azushiwa kufa kwa kuchomwa kisu


Mapema wiki hii kulizuka tetesi kuwa nyota wa reggae/dancehall Shaggy amefariki na kuenea kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii.

Tetesi hizo zilidai kuwa Shaggy alichomwa kisu baada ya kutokea ugomvi kwenye nightclub jijini Los Angeles.Mbaya zaidi mpaka mtandao wa Wikipedia uliupdate historia ya Shaggy kuwa amefariki dunia kwa kuamini rumors hizo.

Mwakilishi wa Shaggy ameuambia mtandao wa TMZ, “[Shaggy] is like a cat with 9 lives … but I can happily report that he’s alive and kicking and in the same building as me right now as we speak.”

Msaada tutani: C-Sir Madini yuko njia panda, hajui aupe jina gani wimbo wake huu!!


ya Avril kuwa kwenye njia panda ya jina gani auite wimbo wake, it seems like si msanii pekee aliyekuwa kwenye dilemma hiyo. Hitmaker wa Kifungo Huru, C-Sir Madini naye yupo kwenye the same boat na anahitaji msaada wako. Msaidie kupendekeza jina la wimbo huu anaotarajia kuuachia hivi karibuni na aliomshirikisha Josefly.

Hemedy: Movie zangu zinaangaliwa sana tangu mfumo wa digitali uanze!!!


Mfumo wa digitali nchini umekuja na faida na hasara zake. Japokuwa hasara ni nyingi, kubwa ni kuwafanya wananchi wengi wenye kipato cha chini kukosa matangazo ya TV kwa kushindwa kununua ving’amuzi, wapo watu wanaonufaika na hali hiyo.

Tangu mfumo huo uanze inasemekana kuwa soko la filamu za Tanzania limeongezeka kwakuwa wananchi wasio na ving’amuzi wamekuwa wakinunua movie za kibongo kwa wingi ili kupoteza muda wawapo nyumbani. Ushahidi wa jambo hilo umetolewa na Hemedy ambaye anasema mfumo wa digitali umeongeza idadi ya warembo wanaompigia simu kusifia movie zake ukilinganisha na zamani.

“Tangia system ya Digital imeanza napokea simu nyingi sana za masista duu wanasifia movie zangu…kitambo walikua wanasema sijui movie zenu,” ametweet Hemedy.

Akijibu swali letu kama anamaanisha kweli, Hemedy amejibu, “true dat….it’s a good thing pia…wanathamini vya home.”