Thursday, October 11, 2012

MKUU WA MKOA WA MBEYA ABAS KANDOLO AMEVUNJA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA NA KUTANGANZA RASMI HALMASHAURI YA RUNGWE ITAKAYO KUWA NA KATA 26 NA KUITANGAZA HALMASHAURI YA BUSOKELO ITAKAYOKUWA NA KATA KUMI NA MOJA.


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbass Kandolo 
Mkuu wa mkoa wa mbeya Abass kandolo amevunja baraza la madiwani wilaya ya rungwe mkoa wa mbeya na kutanganza rasmi halmashauri ya rungwe itakayo kuwa na kata 26 na kuitangaza halmashauri ya busokelo itakayokuwa na kata kumi na moja.
Akiongea na baraza la madiwani mkuu wa mkoa wa mbeya amsema kuwa serikali imeanzisha kifungu (sub_vote) na>7813140 na kutenga fedha kwenye bajet ya mwaka wa fedha 2012/2013 kwa ajili ya halmashauri ya busokelo, yenye jumla ya tsh 12,549,250,889/=
Halmashauri ya rungwe itakuwa ikiongozwa na mkurugenzi noel mahyenga pia halmashauri ya busokelo itakuwa inaongozwa na imelda ishuza aliyeteuliwa kuiongoza halmashauri ya busokelo inayoanza leo kuwahudumia wananchi wa busokelo.
Akitoa saram za mkoa mkuu wa mkoa wa mbeya kandolo amewataka wananchi kufanya kazi kwa bidii na kuchangia shughuri za maendeleo na hili itazizifanya halmashauri kuwa maendeleo zaidi.
Pia amesema haitakuwa na maana kuwa na halmasahauri mbili bila ya kujibidisha kufanya kazi za maendeleo na kukusanya ushuru ili kujiwezesha kujitegemea
Zaidi amewapongeza wananchi wa busokelo kupata huduma za maendeleo karibu na wao
Amewahakikishia kuwa serikali kwa kuzingatia ahadi ya rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania dr jakaya kikwete aliyoitoa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ombi lililotolewa na mbunge wa rungwe masharika prof mark mwandosya katika kiwanja cha tandale na rais aliahidi kuifanya wilaya ya rungwe kuwa na halmashauri mbili rungwe na busokelo na leo ahadi hiyo imetimia kwa kupata halmashauri ya mpya ya busokelo.

Baraza la Madiwani kabla ya kuvunjwa

MKUU WA WILAYA RUNGWE CYPRIAN MEELA AKIONGEA NA MADIWANI

KABLA BARAZA LA MADIWANI HALIJAVUNJWA

No comments:

Post a Comment