Monday, October 15, 2012

ZAMBI AWA MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MBEYA




Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mashariki Godfrey Zambi ameshinda nafasi ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Mbeya.
Zambi kapata kura 888 na kufuatiwa na Allan Mwaigaga ambaye amepata kura 318 na kufuatiwa na Reginald Msomba aliyepata kura 237

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima ndiye alikuwa msimazi wa uchaguzi huu akitangaza matokeo

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mstaafu mkoa wa Mbeya, Nawab Mullah, akimkaribisha mwenyekiti mpya Mh Zambi

Allan Mwaigaga ambaye amepata kura 318 na kuwa mshidi wa pili akiwashukuru wanachama wa ccm katika uchaguzi huo na kusema sasa makudi yavunjwe maadam mshindi kapatikana 

Reginald Msomba aliyepata kura 237. mshindi wa tatu nae pia akiwashukuru wanachama wa ccm katika uwanja wa sokoine jijini mbeya

Mkuu wa mkoa Mbeya Abasi Kandoro kulia katikati chales Mwakipesile kushoto kabisa mwenyekiti mstaafu mulla wakiwa makini kufuatilia matokeo uwanjani hapo mida ya saa sita kamili usiku

wanachama wa ccm wakiwa makini kusikiliza matokeo uwanjani hapo

Mwenyekiti mpya Zambi akipongezwa na mwenyekiti mstaafu Mullah mara baada ya kutangazwa mshindi

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima akimsisitizia jambo fulani mwenyekiti mpya wa ccm mkoa wa mbeya G. Zambi

Mbunge wa Jimbo la Mbozi Mashariki Godfrey Zambi amabaye sasa ni mwenyekiti wa ccm mkoa wa Mbeya akiwashukuru wanachama wa chama hicho kwa kumchagua

No comments:

Post a Comment