Thursday, November 22, 2012

Breaking News: Muigizaji Mlopelo Asemekana Kufariki Dunia



Muigizaji mahiri ambaye alikuwa anatamba katika kundi la Kaole Sanaa Group Mlopelo anasemekana amefariki dunia siku ya leo. Kwa mujibu wa taarifa ambazo pia bongo5 inajaribu kuzithibitisha kutoka kwa mmoja wa wana tasnia ya filamu Pastor Myamba, ambaye naye ametupasha kupata taarifa za kifo chake kupitia ujumbe mfupo wa maneno.
Inasemekana Chanzo cha kifo chake ni maradhi ya muda mrefu.
Mlopelo mara nyingi alikuwa anaigiza kama zezeta la msukule na kujipatia umaarufu mkubwa kutoka kwa wapenzi na tamthilia za kitanzania ambazo mara nyingi zilikuwa zinaonekana kupitia ITV na Channel Ten.
Bongo5 inajaribu kufuatilia habari hii kwa kina zaidi.

No comments:

Post a Comment