Wednesday, January 30, 2013

Lulu aziteka ‘frontpage’ za magazeti ya leo (Jan 30)


Picha za msanii wa filamu Elizabeth Michael maarufu Lulu ambaye jana alitoka nje kwa dhamana, zimeyateka karibu magazeti yote ya Tanzania ya leo.

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemwachia kwa dhamana Lulu aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya kumuua msanii mwenzake wa filamu Steven Kanumba Aprili 7, 2012 bila kukusudia baada ya kukamilisha taratibu zote za dhamana.

Masharti ya dhamana hiyo ni kutakiwa kuwa na wadhamini wawili ambao ni wafanyakazi wa serikali waliotakiwa kutoa shilingi milioni 20 kila mmoja. Mengine pamoja na Lulu kurudisha hati yake ya kusafiria, haruhusiwi kutoka nje ya Dar es Salaam na atatakuwa kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya mwezi.

Magazeti yote ya Kiswahili na Kiingereza a Tanzania yameandika habari hiyo ama kuweka picha za Lulu baada ya dhamana yake kukamilika jana.Picha nyingi zinamuonesha Lulu akilia kwa furaha huku akiwa bega kwa bega na mama yake mzazi.









No comments:

Post a Comment