Wednesday, January 30, 2013

Maoni: TID na Wema Sepetu wapendekezwa zaidi kuiwakilisha TZ kwenye BBA 2013, mnyama asema atachukua fomu



Tarehe 26 tuliandika habari kuhusu Mastaa 10 wanaoweza kuwa wawakilishi wazuri wa Tanzania katika shindano la Big Brother Africa 2013. Katika majina hayo 10, Wema Sepetu, TID, Lisa Jensen na Fezza Kessy ndio walionekana kuwavutia wengi.

Leo kupitia ukurasa wetu wa Facebook tumeendesha kura ya maoni ambapo tumewataka watu wawataje mastaa kati ya hao wanne wanaoweza kuwa wawakilishi wazuri wa Tanzania. Katika kura hizo zaidi ya 800 TID na Wema ndio walioongoza kwa kutajwa zaidi.

Baada ya matokeo hayo tumempigia simu TID kumpa taarifa hiyo aliyoipokea kwa furaha kubwa na kudai kuwa hiyo ni ishara ya jinsi anavyokubalika kwa mashabiki.Tulipomuuliza kama atafikiria kuchukua fomu kwaajili ya kujaribu bahati yake, Top in Dar amesema kwakuwa watanzania wamemtaka afanye hivyo basi ataenda kuchukua.

Tunafanya jitihada kupata msimamo wa Wema pia.Tazama maoni hayo hapa:

http://www.facebook.com/photo.php?fbid=529169297116509&set=a.296410577059050.80456.107179369315506&type=1&theater

No comments:

Post a Comment