Thursday, February 7, 2013

Picha: Rihanna amsindikiza Chris Brown mahakamani



Jana wapenzi waliorudiana rasmi, Chris Brown na Rihanna walionekana wakitoka pamoja nyumbani kuelekea mahakamani jijini Los Angeles.Rihanna alikuwa amevaa sunglasses na mara nyingi alikuwa ameinama chini kuziba uso wake.




Wapenzi hao walisindikizwa na mama yake Chris Joyce Hawkins wakati huu ambao Brown anadaiwa kudanganya masaa ya kazi alizozifanya kwenye jamii kama sehemu ya probation yake kufuatia kesi ya kumpiga Rihanna mwaka 2009.

Wakili wa Brown Mark Geragos na polisi wa Richmond Virginia wamekanusha madai hayo. Akiongea na waandishi wa habari jana Geragos alisema: Sijawahi kuwa na mteja aliyeteswa kama Chris Brown.

Chris akiwa mahakamani


Aliongeza kuwa Rihanna alimsindikiza Brown mahakamani na hajafurahishwa na madai hayo mapya.



Rihanna na Chris walipokuwa wakitoka studio jana Jumatano

Abela: I want to make my country Tanzania proud





Despite the fact that she spends more of her life time in United States, Abela Kibira aka Tanzania’s own as she calls herself on Twitter has never forgotten Tanzania where her father Josiah Kibira was born.

“I want to make my country Tanzania proud and represent them in everything that I do,” she says on Twitter.

She is very talented and very beautiful as well so we hope she will make us proud. She expects to visit Tanzania this April but seems to have a little challenge.

“Yeah despite people not wanting me to I think an extended period of time in TZ is needed for me,” she tweets.

Abela E. Kibira was born on September 22nd, 1989. The first child to her American mother and Tanzanian father,her two cultures intertwined through music. Her first performances were in church, in school programs, and at special events. Growing up in Wayzata, Minnesota she was incredibly active in the choral programs in middle school, and more rigorously in high school. In 2003 her father released his first feature film through his independent film company Kibira Films International, and Abela was featured on the soundtrack for the film.




Young, fresh and ambitious. She has been studying and performing vocal music her entire life. She is currently experimenting with hip hop, hip hop fusion, reggae and alternative styles of music.

She was featured on the soundtrack for full length feature film “Bongoland” released in 2003. “There still are people in the world who think of the United States as the land of milk, honey and no problems, says Josiah Kibira (her father) and he’s determined to set them straight. The Tanzania native, who lives in Plymouth with his American wife and their children, decided to write and direct a drama in a mix of English and his first language, Swahili.” ”

FastJet: ‘Hatujanyang’anywa leseni, tunapiga route kama kawa’ yasema kuna watu wamepanga njama ya kuiangusha!

Kampuni ya ndege ya Fast Jet imezikanusha ripoti kuwa imenyang’anywa leseni yake ya biashara katika nchi kadhaa barani Afrika ikiwemo Tanzania.Kupitia website yake kampuni hiyo imeandika:

Licha ya taarifa za leo kwenye vyombo vya habari, ni biashara kama kawaida hapa fastjet. Madai kuhusu kunyang’anywa leseni ni uongo mtupu. Tunaendelea na safari zetu kutoka Tanzania na tunaendelea kuanzisha safari mpya kama ilivyopangwa.

Hii ni njama/hujuma ‘binafsi’ dhidi ya fstjet katika jaribio wazi lililotengenezwa kuharibu brand na sifa ya Fastjet.Ofisi zetu na matawi yetu bado zipo wazi kwa booking mpya na hakuna refund zozote.

Taarifa rasmi itapatikana masaa machache yajayo.

www.fastjet.com

For further information regarding these reports please read below:

7th February 2013

fastjet plc
(“fastjet” or the “Company”)
Brand Licence

In response to recent misleading press reports, David Lenigas, Chairman of fastjet plc and Chairman of Five Forty Aviation Limited (Kenya) (“Fly540 Kenya”), confirms that there is no valid Brand Licence Agreements, Franchise Agreements or Management Agreements between Fly540 Kenya and Fastjet or any other Fly540 associated Companies in Africa.

Statements made by Don Smith from Kenya, a director of Fly540 Kenya, suggesting he has the right to withdraw the Brand are absolutely wrong and without foundation. The Board of Directors of Fly540 Kenya has never met to even consider this issue.

fastjet wishes to advise the media and our passengers who fly with us throughout Africa in either a fastjet plane, Fly540 plane or Fly540 Africa plane, that we are looking forward to expanding our Low Cost Airline throughout the African Continent..

Flaviana Matata kutokea ndani ya jarida la Marie Claire la Marekani




Kila siku mwanamitindo wa kimataifa Flaviana Matata amekuwa akiendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania kwa kuhusika kwenye masuala makubwa kimataifa. Ni jana tu tuliandika habari ya Flavy kupata shavu la kushiriki kwenye matangazo ya Diesel + Edun.

Hivi karibuni mrembo huyo ataonekana pia kwenye jarida la Marie Claire la Marekani. Jarida hilo la wanawake huandika makala mbalimbali na picha kuhusu fashion, mitindo, urembo, mambo ya wanawake, kazi, afya na mambo mengine.

Kupitia Instagram, Flavy ameshare picha ya akiwa na warembo wengine wa kimataifa kwenye photoshoot ya magazine hiyo na kuandika: hooting for Marie Claire America with @kimiskoo1 (Kim Koo) and @snik1 (Kaya Wilkins).


Kila siku mwanamitindo wa kimataifa Flaviana Matata amekuwa akiendelea kuipeperusha bendera ya Tanzania kwa kuhusika kwenye masuala makubwa kimataifa. Ni jana tu tuliandika habari ya Flavy kupata shavu la kushiriki kwenye matangazo ya Diesel + Edun.

Hivi karibuni mrembo huyo ataonekana pia kwenye jarida la Marie Claire la Marekani. Jarida hilo la wanawake huandika makala mbalimbali na picha kuhusu fashion, mitindo, urembo, mambo ya wanawake, kazi, afya na mambo mengine.

Kupitia Instagram, Flavy ameshare picha ya akiwa na warembo wengine wa kimataifa kwenye photoshoot ya magazine hiyo na kuandika: hooting for Marie Claire America with @kimiskoo1 (Kim Koo) and @snik1 (Kaya Wilkins)

.
Kim Koo

Kaya Wilkins

Flaviana Matata


Madee kuitafuta pombe yake kwenye ngoma mpya




Rapper na member wa Tip Top Connection, Madee amepanga kufanya kitu cha tofauti kwa mwaka huu kwa kuachia ngoma aliyoipa jina, “Pombe Yangu”.

Akizungumza kwenye E-Newz ya EATV kuhusiana na jina la wimbo huo ambalo limezua maswali na utata mkubwa amesema,” Ngoma hii ambayo ipo katika mtindo wa Kwaito ni kwaajili ya ku-party na inaelezea mazingira ya marafiki ambao wanakutana sehemu kwaajili ya kufurahia kinywaji”.

hata hivyo Madee amesisitiza kuwa yeye binafsi huwa hanywi pombe ila anafurahia kukaa mazingira ambayo kuna watu wanaopiga mtungi.

Wednesday, February 6, 2013

Polisi walioitwa kumsaidia Jaydee wamgeuka, waita waandishi wa habari wapate habar




Jana kupitia mtandao wa Twitter mwanadada Lady Jaydee alisimulia kitendo kilimchokera baada ya polisi walioitwa kwenda kumsaidia akiwa kwenye chumba cha hoteli baada ya kuzidiwa ambao waliamua kuwapigia simu waandishi wa habari za udaku waje wapate picha na habari.

“Police mnatumwa kuja kuni rescue mgonjwa Hotel Room, mnaita waandishi waje kuchukua story! Hamjanitendea haki, nimesikitishwa,” alitweet Jaydee.

“Nawaambia I can’t walk wananilazimisha shuka watu watakubeba gari tumepaki nyuma. Kumbe camera ziko chini huko zinangoja.”

Akijibu swaliu la Bongo5 lililouliza kama waandishi hao walipata walichokitaka Jaydee alijibu, “I told them walete doctor humo hotel room kama hawaezi waondoke. Hotel staff told me nsishuke kuna camera chini.”

“Mwenyewe nashangaa hawakuwa wanajali mimi kupata nafuu bali maslahi. Hakuna utu hapo.”

Alimalizia kwa kuandika, “Hamtujali, na hamjali lolote. Kila mtu ana shida zake ila msichukulie advantage kutunyima haki zetu za msingi. Nimeumia sana!

Hata hivyo Jaydeea alidai kuwa kwa sasa anaendelea vizuri ingawa hatukuweza kufahamu alikuwa hoteli gani na wapi pamoja na tatizo lililokuwa likimsumbua.

Pole Jide.

Tuesday, February 5, 2013

Zola D kuanzisha kipindi cha TV cha mazoezi!



Hivi karibuni Bongo5 ilichat na rapper na bondia nchini Tanzania, Zola D ambaye alisema ana mpango wa kuanzisha kipindi cha TV.

“Now nina mpango wakuanzisha kipindi cha TV pia na kurusha video zangu za mazoezi kwenye Youtube ili kila mtu alie nyumbani aweze kufanya mazoezi sio mpaka uingie gym, “ alisema Zola.

“Mimi siendi gym kufanya mazoezi nafanya home pia gym naenda kama nina game ya boxing,ili niweze kufundishwa na mwalimu mbinu mbali mbali za mapigano na ushindi.”
Zola akiwa na P-Funk

Akijibu swali la ni vipi ameweza kuujenga mwili wake kiasi hicho, Zola amesema, “Mwili wangu nimeujenga toka miaka mingi sana sasa nina miaka 18 tokea nimeanza kufanya mazoezi ndio maana unaweza kuona mwili wangu umejengeka sana kuliko watu wengine hapa Bongo. Pia mazoezi ninayofanya ni mazoezi ya mapigano na mazoezi ya kujenga nguvu kama push up kukimbia,kuruka kamba,na kufanya swimming sababu napenda sana mazoezi na ndio starehe yangu kubwa,pia nafanya mazoezi kila siku ndio chakula cha maisha yangu,so kila siku nazidi kugain na kuongezeka.”

“Mazoezi yananisaidia sana kwenye afya yangu coz sijaumwa malaria huu ni mwaka wa 4 pia mafua kifua nk,coz ukifanya mazoezi damu inakuwa na nguvu sana,”aliongeza.

Hata hivyo Zola amesema hana pambano lolote hivi karibuni na kuongeza kuwa mchezo wa ndondi kwa Tanzania haulipi.

“Game za Bongo hakuna pesa kabisa ni kuumizana tu promoter wenyewe njaa tu, promoter hana hata baiskeli. Nia yangu ni kupigana ngumi za nje na kuitangaza Tanzania.Nipo tayari kupigana na bondia yoyote mkubwa wa dunia coz najua nina kipaji cha sports pia napenda sana kupigana nikitoka damu ndio naskia raha sana najiona mimi ndio mwanaume.”
Zola na Mad Ice


Kuhusu kuzichapa kiukweli na Mad Ice ambaye pia ni bondia na ameigiza kwenye video yake ya Knock OUT, Zola amesema Ice ni mtoto mdogo.

“Mad ice hawezi kupigana na mimi,pia mimi ni mwalimu wake namfundisha boxing. Nawaomba watanzania wazidi kuniombea dua niweze kutimiza ndoto zangu za kupigana level za kimataifa,muziki wangu level za kimataifa na michezo yangu mingine kama kukimbia mita 100, mita 200,kuruka viunzi,kucheza rugby, kupigana boxing mixed martial arts.”