Thursday, October 11, 2012

DIAMOND PLATNUMZ APIGA KAMPENI NGORONGORO CRATER

Diamond Platnam'z

SANII wa muziki wa kizazi kipya,Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amewataka watanzania kulipigia kura bonde la Ngorongoro kuwa moja ya maajabu saba ya Afrika na pia kujenga tabia ya kutembelea vivutio vya utalii vya ndani.
Akizungumza mjini Ngorongoro, Diamond ambaye alikuwa huko kujionea bonde hilo ambalo ni la kipekee ulimwenguni, amesema hakuwahi kufikiria kwamba kuna sehemu nzuri ambayo hata watanzania wanaweza kwenda kutembea na kujionea vivutio vilivyopo.
“Hii ni mara yangu ya kwanza kufika hapa, lakini kwa kweli nimeshangazwa na jinsi palivyo pazuri, wanyama, mito ambayo inapita huku chini, mi huwa naona kwenye televisheni tu katika kile kipindi cha National Geography cha DSTV lakini sikujua kama mambo haya yapo kweli kwetu.
“Nawaomba watanzania wenzangu waweze kutembelea Ngorongoro na vivutio vyetu vya utalii kwa sababu kuna mengi ya kujifunza, leo kama isingekuwa Afrika sidhani kama kungekuwa na kipindi kama National Geography, na gharama za kuja huku si kubwa, hatupaswi kuogopa, hivi ni vitu ambavyo vinawezekana kabisa suala ni kujipanga,” amesema.
Amesema wenzetu kutoka Ulaya wamekuwa wakijipanga kuweza kutembelea sehemu Fulani jam bo ambalo linawafanya waweze kutembelea nchi nyingi kufanya utalii.
“Pamoja na kuja kupunguza mawazo lakini sehemu kama hii inasaidia kuelemisha, mwito wangu kwa watanzania wenzangu, mashule hata vyuo waweze kuja hapa, inakuwa rahisi zaidi kumfundisha mtoto kuhusu Simba, Twiga, au bonde la Ngorongoro kwa kumuonyesha hiki kiko hivi, nadhani kama watoto watakuwa wanasoma kwa vitendo hawawezi kushindwa mitihani yao kwa sababu kumbukumbu inabaki kichwani kwa kile walichokiona,” amesema.
Msanii huyo alikwenda Ngorongoro baada ya kumalizika kwa tamasha la Fiesta ambapo alikuwa mmoja wasanii waliofanya vizuri. Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ilimualika Diamond huko. Ngorongoro ni moja kati ya vivutio vya Tanzania vinavyotakiwa kupigiwa kuingia katika maajabu saba ya Afrika
Diamond plutnim'z

OFFICIAL RELEASE: C-SIR MADINI "PAIN KILLER" (Audio & Lyrics))

Hello mambo vipi




Please pokea wimbo mpya wa Msanii C-SIR MADINI (Sisa) ambayo leo ndio tunai release rasmi kuanza kuchezwa katika radio stations. Video tayari ilitoka siku mbili zilizopita.

The story behind the existence of this song, ni kwamba kwanza ni wimbo ambao umeandikwa na kurekodiwa siku moja ilikuwa mwezi may 2012, baada ya hapo kazi ya umaliziaji wa beat pamoja na mixing ikaendelea kwa takriban wiki 2.

Idea ya wimbo huu, title na lyrics zote zimeandikwa na kidbwoy, na zina base katika chembechembe za true story zinazomhusu muandishi wa wimbo huu.

Maana ya wimbo huu ni kwamba, C-sir amepata kitulizo cha moyo wake ulioumizwa na mpenzi alietangulia, hivyo baada ya kumpata mtu alieamini kuwa ndio tulizo la moyo wake, huyo ndio akawa Pain Killer yake, lakini ni tofauti na pain killer zote unazozifahamu ambazo mara nyingi huwa zina uchungu wakati wa kumeza. Tofauti ya Pain Killer ya C-sir na Pain Killer za maumivu ya kichwa ni kuwa hii ni "PAIN KILLER/TAMTAM", licha ya kumtibu lakini bado ni tamu.

Hii ni ngoma ya 3 kwa C-sir Madini kuachia, baada ya KIFUNGO HURU iliyotoka kama single ya kwanza mwaka jana, iliyofuatiwa na NISHIKE MKONO aliyoitoa mwezi January mwaka huu 2012.

Arist Nick name: C-SIR MADINI (Sisa)
Real Name: PETER MPONEJA
Birthdate: 07th may 1992
New release: PAIN KILLER
Written by: Kid bwoy
Produced by: Kid bwoy
Studio: Tetemesha Records


“PAIN KILLER” Lyrics by C-SIR MADINI (SISA)
Written by: Kid bwoy
Produced by: Kid bwoy
Tetemesha Records, 2012

Intro:
We ndo ma painkiller
Ooh ma ma ma ma, oooh
Tam tam oooh, yako tam tam
Tam tam oooh, yako tam tam

Verse 1:
Mwanzo aliniona kwenye twitter, kabla jina sijalipata,
Kifungo huru ilimvuta, nishike mkono ikafata,
Ana sifa nyingi kaumbika, sauti ka mtoto amepita,
Top ten yama miss wa bongo, namba moja ashaipata,

Bridge :
Nikikatiza nae kitaa watu wote ndalile, oooh wanabaki ooooh,
Usijaribu fata hii asali yangu ndalile, oooh utalia oooooh,x 2

Chorus:
Ye ndo pain killer yangu, moyo hauna utata,
Yeye ndo tekila yangu, siogopi ukata,
Ye ndo medulla yangu, stress zikinikamata,
Ye ndo cellular yangu, nilipo utamkutaaa,
Aiyaa taiyaaaa, aaaaaaaah x2

Verse 2:
Kama ni nguo ye si mtumba kipya kinyemi wadananda ndo mjue, hai
Tena nitafuga mbwa nshaweka fensi wadoezi msinijue, hai
Kama ni nguo ye si mtumba kipya kinyemi wadananda ndo mjue,
Tena nitafuga mbwa nshaweka fensi wadoezi msinijue,
Una create attention, attention lazima watupishe, hai
Unawaongezea tention, tension lazima watupishe, hai
Una create attention, attention lazima watupishe,
Unawaongezea tention, tension lazima watupishe,
Bridge :
Nikikatiza nae kitaa watu wote ndalile, oooh wanabaki ooooh,
Usijaribu fata hii asali yangu ndalile, oooh utalia oooooh,x 2

Chorus:
Ye ndo pain killer yangu, moyo hauna utata,
Yeye ndo tekila yangu, siogopi ukata,
Ye ndo medulla yangu, stress zikinikamata,
Ye ndo cellular yangu, nilipo utamkutaaa,
Aiyaa taiyaaaa, aaaaaaaah x2

Verse 3:
We ndo ma pain killer, aaaaaaah
We ndo ma heart desire, aaaaaaaah

Pilipili pili yako tam tam ooooh, yako tam tam
pili pili yako tam tam ooooh, yako tam tam
Nyanya chungu yako tam tam ooooh, yako tam tam
Nyanya chungu yako tam tam ooooh, yako tam tam x2

Chorus:
Ye ndo pain killer yangu, moyo hauna utata,
Yeye ndo tekila yangu, siogopi ukata,
Ye ndo medulla yangu, stress zikinikamata,
Ye ndo cellular yangu, nilipo utamkutaaa,
Aiyaa taiyaaaa, aaaaaaaah x2

Outro:
Tam tam oooh, C-sir Madini
Tam tam oooh, Tetemesha
Tam tam ooh, yako tam tam
Da nda da da nda da danda da da nda da
Da nda da da nda da danda da da nda da, uuh
Da nda da da nda da danda da da nda da, uuh
Da nda da da nda da danda da da nda da...
Aaaaaaaah aaaaaaah aaaaaaah
END  

MKUU WA MKOA WA MBEYA ABAS KANDOLO AMEVUNJA BARAZA LA MADIWANI WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA NA KUTANGANZA RASMI HALMASHAURI YA RUNGWE ITAKAYO KUWA NA KATA 26 NA KUITANGAZA HALMASHAURI YA BUSOKELO ITAKAYOKUWA NA KATA KUMI NA MOJA.


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbass Kandolo 
Mkuu wa mkoa wa mbeya Abass kandolo amevunja baraza la madiwani wilaya ya rungwe mkoa wa mbeya na kutanganza rasmi halmashauri ya rungwe itakayo kuwa na kata 26 na kuitangaza halmashauri ya busokelo itakayokuwa na kata kumi na moja.
Akiongea na baraza la madiwani mkuu wa mkoa wa mbeya amsema kuwa serikali imeanzisha kifungu (sub_vote) na>7813140 na kutenga fedha kwenye bajet ya mwaka wa fedha 2012/2013 kwa ajili ya halmashauri ya busokelo, yenye jumla ya tsh 12,549,250,889/=
Halmashauri ya rungwe itakuwa ikiongozwa na mkurugenzi noel mahyenga pia halmashauri ya busokelo itakuwa inaongozwa na imelda ishuza aliyeteuliwa kuiongoza halmashauri ya busokelo inayoanza leo kuwahudumia wananchi wa busokelo.
Akitoa saram za mkoa mkuu wa mkoa wa mbeya kandolo amewataka wananchi kufanya kazi kwa bidii na kuchangia shughuri za maendeleo na hili itazizifanya halmashauri kuwa maendeleo zaidi.
Pia amesema haitakuwa na maana kuwa na halmasahauri mbili bila ya kujibidisha kufanya kazi za maendeleo na kukusanya ushuru ili kujiwezesha kujitegemea
Zaidi amewapongeza wananchi wa busokelo kupata huduma za maendeleo karibu na wao
Amewahakikishia kuwa serikali kwa kuzingatia ahadi ya rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania dr jakaya kikwete aliyoitoa katika kipindi cha kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ombi lililotolewa na mbunge wa rungwe masharika prof mark mwandosya katika kiwanja cha tandale na rais aliahidi kuifanya wilaya ya rungwe kuwa na halmashauri mbili rungwe na busokelo na leo ahadi hiyo imetimia kwa kupata halmashauri ya mpya ya busokelo.

Baraza la Madiwani kabla ya kuvunjwa

MKUU WA WILAYA RUNGWE CYPRIAN MEELA AKIONGEA NA MADIWANI

KABLA BARAZA LA MADIWANI HALIJAVUNJWA