Sunday, December 2, 2012

Video: Jua walichoongea Dude na Sharomilionea kabla ya kupoteza maisha



Mwigizaji Dude amefunguka kuhusu maongezi yake na marehemu Sharo Milionea kabla ya ajali kutokea, msikilize hapa.

wimbo wa all stars kama kumbukumbu ya SHARO MILLIONEA

Fid Q amtambulisha dogo aliyemfunda kwa miezi 9

Fid Q


Mwanamuziki mkongwe wa Hip hop Fid Q , almaarufu kama Ngosha the Don, amesema ameamua kumchukua mwanafunzi mmoja na kumfundisha Muziki ili mwanafunzi huyo aweze kupambana na ushindani mkubwa uliopo kutoka kwa wasanii mbali mbali kwenye Muziki.

Akiongea kupitia kituo kimoja cha Radio leo jijini Dar-Es-Salaam, Fid Q alisema anaona fahari kuwa msanii anayetoa fursa kwa vijana badala ya wao (vijana) kumtegemea kwa kolabo ama pesa lakini kwa kuwafunda yeye mwenyewe wataweza kujihudumia wenyewe katika siku za baadae.

Fid Q amekuwa mfano mzuri sana wa kuigwa katika ubunifu na moyo wa kujitolea, na katika siku za hivi karibuni kupitia mahojiano tuliyoyafanya naye msanii Stamina, alionyesha kumkubali sana Fid Q, na kusema ni mtu anayemtegemgea kwenye Muziki wa Hip Hop kwa sababu anamuona kama ni nguzo na msingi wa Hip Hop hapa bongo.

Stamina alisema “kama kuna msanii ambaye ninamkubali sana, basi ni Fid Q , kwani ni msanii pekee aliyesoma vitabu vingi sana ndiyo maana haishiwi mashairi, pamoja na uwezo wake wa kuchana.
Aidha Fid Q alisema mwanzoni aliwawachukua vijana 6 ambao bado walikuwa hawajakomaa, kwa hiyo akawafanya kama wanafunzi na kuwafundisha muziki, na hatimae sasa mmoja wao amemaliza masomo na na kuwa msanii ambaye aliyeiva kimuziki.

Fid Q alisema “nimeamua kuwafundisha vijana muziki ili wawe na uwezo kama wangu na kuwapa fursa katika maisha yao kwa sababu ni vigumu sana mtu kumpa kazi ambayo itamsaidia kimaisha ila ukimpa fursa utamsaidia sana kuliko kumpa pesa. Alimalizia.

Saturday, November 24, 2012

Chezea Tuzo; AY Ampiku Diamond Kufanya Kolabo Na J Martins



Kwa wale ambao walikuwa wakifuatilia kwa karibu, habari za msanii Diamond kwa kipindi kirefu cha mwaka huu watapata kushangaa nini kimetokea kwa kolabo yake na msanii J Martins ambayo amekuwa akiitangaza mara kwa mara huko nyuma.


Well kwa sasa inaonekana msanii huyo kutoka Nigeria atafanya kazi na msanii aliyepata tuzo ya video bora Afrika Mashariki kupitia Kolabo na wasanii wa Kenya Sauti Sol, Ay na swahiba wake wa karibu Mwana FA.
Kwa mujibu wa tetesi za chinichini, mipango yote ya kolabo hiyo imeshaiva na pengine kazi hiyo ikakamilika siku si nyingi.
Well tusubiri na tuone yatakayojiri.

Sajuki Kuwashukuru Watanzania Live Kwa Mara ya Kwanza Iringa


KATIKA kutoa shukrani kwa Watanzania wote waliowajibika katika kuhakikisha wanamsaidia mwigizaji na mtayarishaji mahiri wa filamu kutoka Swahiliwood Juma Kilowoko ‘Sajuki’ kupatiwa matibabu kutokana na maradhi ya tumbo na kwenda kutibiwa Nchini India na kupona, kampuni ya Wajey Film Company imeandaa tamasha kubwa la shukrani.
Ni tamasha la aina yake kutokana wa wadau wafilamu na Watanzania kwa ujumla kufurahia kurudi kwa sajuki katika hali yake ya mwanzo, Stara alisema onyesho hilo litafanyika kwa ajili ya kukusanya fedha zitakazopelekwa kwa wasanii wanaosumbuliwa na maradhi na kukosa matibabu alisisitiza mratibu huyo.
Bongo5 iliongea na mmoja wa wakurugenzi wa kampuni hiyo mahiri katika utengenezaji wa filamu, Wastara Juma ‘Stara’ amesema kuwa baada ya mumewe Sajuki kupata matibabu anatumia fursa hiyo katika kuwashukru watanzania waliojitoa kwa hali na mali katika kufanikisha matibabu hayo.
kama familia hatuna cha kuwalipa watanzania kwa moyo wao wa upendo walioonyesha kwetu, katika kipindi kigumu na majaribu wakati Sajuki akiwa anaugua, si rahisi kumfikia kila mtu kwa wakati mmoja lakini kwa njia ya tamasha hilo tutawafikia, tunawapenda watanzania mungu awabariki sana,”anasema Wastara.
Tamasha hilo linatarajia kufanyika siku ya jumapili Tarehe 25/11/2012 katika uwanja wa Samora huku wasanii wa muziki wakitumbuiza kwa nguvu Mzee Yusuf, Linah, H. Baba na mchekeshaji Kitale ataimba burudani kubwa ni pale mechi kali itakapopigwa kati ya wasanii nyota wa filamu kutoka Bongo movie na timu kali ya watangazaji wa redio zote mkoani Iringa.

Ni kweli Keri Hilson aliidiss Afrika kwa kutuita starving Africans?

Huenda Keri Hilson akaja Tanzania na Kenya katikati ya mwezi ujao (December) akiwa tayari amewakera waafrika kwa tweet yake ambayo yeye anasema hakuiandika. Tweet hiyo inayotuponda waafrika kuwa tunakufa na njaa.

Katika tweet hiyo Keri aliandika, “IT’S THANKSGIVING ! Just did that 19 hour flight back from Ghana and most definitely am going to eat like a pig for the starving Africans.”

Tweet hiyo iliamsha hasira kubwa wa waafrika waliochukizwa na kitendo cha msanii huyo kulidharau bara la Afrika kiasi hicho.

Jana imemlazimu msanii huyo kukanusha kuandika tweet hiyo kwa madai kuwa kuna mtu aliitengeneza kwa kutumia program ya photoshop ili kumkosanisha na waafrika.

“Wow. People actually believe I’d say that? I woke up & saw a fake photoshopped tweet abt me dissing Africa?! C’mon man. Really? Disgusting.

“REALLY didn’t wanna spend any part of my day combating foolishness But I simply cannot hv u doubting my sincerity abt my love for Africa!”

“And for those still skeptical, I wasn’t even in Ghana this trip. They didn’t even have the facts right to make it believable.”

Tumwamini nani?

Avril wa Kenya kuja na ear/headphones zake



Msanii wa kike wa nchini Kenya, Avril ameamua kuonesha kuwa biashara ya headphones inaweza kufanywa na msichana pia kwa kuanzisha aina ya ear/headphones zake ambazo kama zikiwa na ubora mzuri huenda kwenye soko la Afrika Mashariki zikatoa upinzani kwa zile za Dr Dre Beats By Dre.

Hata hivyo mradi wake huo utapewa shavu na wizara ya elimu ya juu, sayansi na teknolojia ya nchini Kenya.

Ear phones hizo zitajulikana kama Gs N Fs na zitakuwa sehemu ya mradi wa kuwainua vijana wenye vipaji na mawazo kuhusiana na teknolojia ambao hawana rasilimali za kuendeleza vipaji vyao.

Picture of the day: AY akipokelewa airport kama kiongozi wa nchi




Kwa kazi aliyoifanya kwenye CHOMVA 2012, AY anastahili mapokezi kama haya. Welcome back home boy.